Saturday 5 March 2022

JUHUDI ZA KUPIGA VITA UVUVI HARAMU KWA NJIA SHIRIKISHI YA JAMII YAANZA KUZAA MATUNDA:

Wanakijiji wa kijiji cha Stahabu Wilayani Pangani Mkoani Tanga watoa mfano wa kuigwa kwenye CFMA ya USTASAKI  kwa kujikita zaidi kwenye uvuvi wa madema na kuachana na aina nyinginezo za uvuvi haramu uliokuwa tishio kwa maeneo hayo licha ya ugumu wa maisha unaowakabili.

Juhudi mbalimbali za uelimishwaji juu ya uvuvi endelevu zinazotolewa na taasisi mbalimbali kwa njia shirikishi ya jamii  Wilayani humo zaanza kuzaa matunda hii ni baada ya kuwashuhudia mabadiliko na jitihata zilizoonekana miongoni mwa wanajamii hawa,wake kwa waume wakijishughulisha zaidi na shughuli za utengenezaji madema ikiwa kama moja kati ya mitego yao tegemezi ya shughuli zao za uvivi za kila siku.

Hii imeonekana siku ya Alhamisi mwakilishi wa AAS alipowatembelea bila taarifa na kuwakuta wakifanya shughuli hizi na kufanya mahojiano nao kwa muda mfupi.


Wito na ushauri toka kwa Jamii hizi:

  • Waungwe mkono ktika kuhakikisha jitihada hizi zina zaa matunda na pia zinakuwa endelevu kwa manufaa ya kizazi cha sasa na kichacho.
  • Elimu ya zana na uvuvi endelevu iendelee kutolewa zaidi ili kutokomeza kabisa uvuvi haramu.
  • Vikundi mbali mbali vya wavuvi wawezeshwe kupata zana bora za uvuvi zenye kuzingatia suala zima la uvuvi endelevu.
  • Ushirikishwaji wa jamii uzidishwe hususani kwenye mbambo mbalimbali ikiwemo mikakati ya kulinda na kutunza rasilimali zao ili kutia mchango wao.  


 Omary ni moja kati ya vijana wakazi wa kijiji hichi,pia ni moja kati ya vijana wenye moyo wa kujituma kuhakikisha uhifadhi unatekelezwa hususani katika jamii yake,pia hakuwa alikuwa mstari wa mbele katika utekelezaji wa zoezi hili.

Saturday 3 April 2021

UVUNAJI NA UUZAJI WA SAMAKI AINA YA KAMBALE:

Ndugu Mnyema Mfugaji wa samaki aina ya kambale anatarajia kuvuna  anatarajia kuvuna samaki wake hivyo anayofuraha kuwaalika wadau wote hususani wachuuzi kwenye shamba lake anapofugia.

Eneo :Kibaha kwa Mfipa
 
Kwa ufafanuzi zaidi kuhusiana na bidhaa na mengineyo kumhusu Mnyema tumia mawasiliano haya:

namba za simu: +255716879793
                           +255779763434 

Karibuni sana!

 

MISITU YA MIKOKO NA IKOLOJIA YA VIUMBE BAHARI:


  • Je unaelewa nini kuhusu misitu ya mikoko? (Tujifunze pamoja)

Misitu ya mikoko ni misitu isiyopukutisha majani kimsimu(evergreen forests)inayopatikana katika ukanda wa mwambao katika eneo la bamvua kubwa na dogo(high and low tides)yenye uwezo wa kuhimili na kukua katika mazingira ya maji ya chumvi.

Ø  Misitu hii hustawi vizuri katika maeneo ya maingilio mito inapokutana na bahari.Ndani ya misitu ya mikoko kuna aina mbalimbali za mimea ,wanyama na wadudu.

 

Ø  Mfumo wa mikoko (Mangrove ecosystem) unahusisha eneo kati ya usawa wa maji ya bahari  wakati wa maji mafu,na usawa wa maji bahari wakati wa bamvua kuu,eneo ambalo lina maji,udongo,miti,wanyama pamoja na viumbe vingine vidogovodogo.

 

 

 

AINA ZA MIKOKO:

v  Kunaaina zipatazo zaidi ya 75 za mikoko ulimwenguni kote,hata hivyo katika nchi zetu za Afrilka Mashariki tuna takrini aina 8 za mikoko ambazo ni:

  1.        Mkandaa(Ceriops tagal)
  2. .       Msinzi (Bruguiera gymnorhiza)
  3. .       Msikudazi au Mkingu (Heritiera Littoralis)
  4. .       Mpia (Sonneratia alba)
  5. .       Mkaka au Mkoko(Rhizophora mucronata)
  6. .       Mkomafi (Xylocarpus granatum)
  7. .       Mchu(Avicennia marina)
  8. .       Mkandaa dume(Lumnitizera racemosa)

 

Ø  Kwanini mikoko inaweza kustawi kwenye maji ya chumvi?

Jibu rahisi: Miti ya mikoko inaweza kustawi katika eneo lenye maji ya chumvi tofauti na miti mingine kwakuwa ina maumbile ya kipekee yanayoiwezesha kupambana na hali hiyo ngumu ambayo kwa mimea mingine ingekufa

 

UMUHIMU WA KUHIFADHI NA KUTUNZA MISITU YA MIKOKO:

Umuhimu wa faida za mikoko unaweza kugawanywa katika sehemu kuu mbili yaani

Faida zinazotokana na mazao ya misitu faida za moja kwamoja na faida za kimazingira zisizo za moja kwa moja;

  1. Nguzo za mikoko kwaajili ya ujenzi wa nyumba
  2. Ngozo za mikoko kwaajili ya biashara
  3. Mbao kwaajili ya samani na ujenzi wa vyombo vya usafiri wa majini(Mashua na majahazi)
  4. Magogo kwa kuchongea mitumbwi,mzinga ya nyuki ,vinu n.k
  5. Kuni
  6. Matunda na majani kwaajili ya dawa
  7. Majani kulisha mifugo (Mbuzi)

 

 

FAIDA ZISIZO ZA MOJA KWA MOJA (FAIDA ZA KIMAZINGIRA):

  1. Mikoko huzalisha na kuzunguusha virutubisho,hivyo hutumika kama chanzo cha chakula kwa mimea na wanyamayakiwemo matumbawe na majani bahari ambayo ni muhimu sana kwa upatikanaji wa samaki.
  2. Mikoko hukinga fukwe za bahari na mito dhidi ya momonyoko wa udongo unaosababishwa na mawimbi.
  3. 3.       Kupunguza kasi ya upepo na hivyo kuzuia au kupunguza vimbunga. 
  4. 4.       Kutumika kama chujio la kupunguza kasi ya udongo unaotoka juu unaoletwa na maji ya mito na mvua na hivyo kuzuia matumbawe na majani ya bahari yasifunikwe na tope jambo ambalo lingesababisha yafe. 
  5. 5.       Hupunguza nguvu ya sumu ya mabaki ya viwandani yanayotupwa baharini.
  6. 6.       Kutumika kama mojawapo ya vivutio kwa watalii
  7. 7.       Kutumika kama mojawapo ya maeneo muhimu ya utalii na mafunzo
  8. 8.       Maeneo muhimu ya matambiko(kwa kibibi/shamba la bibi)  
  9. 9.       Mikoko ni sehemu muhimu ya kuzaliana,kulishia na kulelea aina mbali mbali za samaki,hivyo kuwepo kwa misitu ya mikoko ni muhimu kwa maendeleo ya kazi za uvuvi.
  10.  10.   Ndani ya misitu ya mikoko hupatikana aina mbalimbali za wa nyama kama vile mbega,kima,tumbili,nguruwe,viboko n.k.
  11. 11.   Wavuvi hupata chambo cha kuvulia samaki ndani ya mikoko
  12. 12.   Mikoko hutumika kutengenezea mitego ya samaki pamoja na maboya kwaajili ya uvuvi

 

 

Thursday 18 July 2019

UMUHIMU WA UFUGAJI WA KUKU WA ASILI (KIENYEJI)

     KUKU WA ASILI(KIENYEJI)     


    Ufugaji wa kuku wa Asili ni jambo lisilo geni katika kaya zetu hapa nchini ni kuku wanaopendwa kufugwa na kuliwa na watu wengi kutokana na uasili wake. Ni dhahiri kwa sasa kuku wa asili(kienyeji) wamekuwa ghali na wanathamani kuliko kuku wa kisasa.

   Kuku hawa wa asili(kienyeji) kuna wanaofuga kwa minajili ya mayai,nyama ama kwa lengo la mradi wa biashara na kujipatia riziki zao.


Kuku wa Asili(kienyeji)

FAIDA NA CHANGAMOTO ZA UFUGAJI WA KUKU WA ASILI(KIENYEJI)


Ufugaji wa kuku wa asili unamanufaa mengi kwa mfano;kuku hutumia eneo dogo kuliko wanyama wengine wa kufugwa,pia hutumia chakula kidogo hivyo ufugaji unaweza kuendeshwa bila kutumia mtaji mkubwa.

  Hizi ni baadhi ya faida na changamoto za ufugaji wa kuku wa asili(kienyeji);

                          Faida za ufugaji wa kuku wa asili

  • Gharama nafuu za kuanzisha na kuendesha mradi wa kuku wa asili.
  • Chanzo cha kipato -mfugaji upata fedha akiuza kuku au mayai.
  • Chanzo cha ajira- ufugaji wa kuku hutoa ajira kwa jamii
  • Nyama ya kuku ni kitoweo kitamu kinachopendwa na kila mtu.
  • Kiini cha njano cha yai kinaweza kutumika kutengenezea mafuta ya nywele.
  • Kuku wa kienyeji anasaidia kusafisha mazingira kwa kula wadudu na kuongeza rutuba kwa mbolea inayotokana na kinyesi cha kuku ambacho hakina kemikali.
  • Mayai huweza kutumika kwa tiba
  • Manyoya yake huweza kutumika kwa mapambo
  • Tangu enzi jogoo amekuwa akitumika kutukumbusha muda/wakati hasa wakati wa alfajiri pale anapowika


               Changamoto za ufugaji wa kuku wa asili

  • Magonjwa kama mdondo na ndui huathiri ufugaji wa kuku.
  • Wezi,wanyama na ndege hushambulia kuku.
  • Ukosefu wa mabanda bora ya kuku
  • Ukuaji taratibu iwapo watakosa lishe nzuri
  • Ukosefu wa chanjo kwa wakati huweza kuathiri ukuaji wa kuku au kuku kupata magonjwa kwa haraka.

             Baadhi ya magonjwa yashambuliayo kuku wa asili;
  • Kideri/mdondo
  • Ndui ya kuku
  • Kipindukipindu cha kuku
  • Mafua ya kuku
  • Homa ya matumbo
  • Kuhara damu
  • Wadudu kama viroboti,chawa,utitiri, kupe wa kuku.

   Pamoja na sifa hizo na changamoto za ufugaji wa kuku wa asili ni muhimu kuku hao wakapewa matunzo mazuri wawekwe kwenye mabanda mazuri na imara, Pia wapewe maji na chakula cha kutosha pia kuwapa chanjo kwa wakati za kuzuia magonjwa mbalimbali...   

Thursday 28 February 2019

UJENZI WA BWAWA LA KUFUGIA SAMAKI

UJENZI BORA WA BWAWA LA SAMAKI

   Ni jambo muhimu sana kuchagua eneo zuri kwa ajili ya ujenzi wa bwawa la samaki ili kufanikisha na kurahisisha kwa urahisi kazi ya kufuga samaki. Si kila eneo la ardhi hufaa kwa kazi ya kufuga samaki. 

 Bwawa linaweza kuchimbwa kwa mkono au kwa mashine, njia zote mbili ni sahihi isipokuwa kama bwawa ni kubwa au unakusudia kufuga kibiashara ni vema ukatumia mashine kwa sababu mashine inafanya kazi kwa haraka na hivyo kumaliza mapema, pia ufanisi wake unakuwa ni mkubwa ukilinganisha na na ufanisi wa bwawa linalochimbwa kwa mkono.

                                             Ujenzi wa Bwawa la Samaki

             SIFA ZA ENEO LA KUJENGA BWAWA LA KUFUGIA SAMAKI


Kwa Bwawa la kusakafiwa kwa udongo wa mfinyanzi hizi ni baadhi ya sifa muhimu sana za kuzingatia katika chaguzi sahihi la eneo:-


➧Liwe karibu na chanzo cha maji salama.

➧Liwe kwenye eneo lenye udongo wa mfinyanzi kwa sababu hauruhusu maji kunywea kirahisi.

➧Liwe katika eneo lenye mteremko kidogo (si lazima sana) ili uwezeshe maji kutiririka kutoka na kuingia bwawani.


Kwa Bwawa la kusakafiwa kwa simenti hizi ni baadhi ya sifa pia muhimu sana za kuzingatia katika ujenzi katika eneo husika:-


➧Liwe na karibu na chanzo cha maji salama.

➧Liwe katika eneo lenye udongo wa mfinyanzi (si lazima sana), uwiano kati ya mchanganyo wa simenti,mchanga na maji wakati wa kutengeneza bwawa la samaki lililo sakafiwa kwa simenti.
            
➧Ni muhimu sana kwa kiwango cha simenti,kokoto kuwa kikubwa zaidi ya kiwango cha                       mchanga na maji ili kuepukana na tatizo la bwawa kupoteza maji kwa mda mfupi.


       KANUNI NA TARATIBU ZA UTENGENEZAJI WA BWAWA LA KUFUGIA SAMAKI

 Ili uweze kufanikwa katika ujenzi bora wa bwawa la kufugia samaki unapaswa kufuata kanuni na taratibu zote katika ujenzi huo.

⥈BWAWA LA UDONGO

Kwa Bwawa la udongo unapaswa kufuata kanuni na taratibu hizi ili uweze kutengeneze bwawa zuri na lenye viwango:-

➧Chagua eneo zuri lenye sifa.

➧Pima udongo.

➧Pima maji.

➧Fanya usafi wa eneo la kujengea bwawa lako (ondoa visiki na vikwazo vinginevyo).

➧Fanya vipimo vya ukubwa wa bwawa lako kulingana na mahitaji yako na ukubwa wa eneo                 lako.
           
➧Zingatia unapofanya vipimo kumbuka kwa kila sqm 1ya bwawa lako utapandikiza samaki                    watatu.

                                     
 Pandikiza majani ya kutosha kwenye kuta.kingo na migongo ya bwawa lako ili kuimarisha bwawa lako lisiharibike kirahisi na mmonyoko wa udongo. Hakikisha unashindilia vizuri kuta,kitako na migongo ya bwawa lako (tumia vitu vizito vya kushindilia ili kuiamarisha zaidi).

 Zoezi hili litafanywa kwa muda wa wiki mbili mpaka tatu likiambatana na zoezi la kumwagilia maji kwa kiasi kidogo sana kwenye kuta ili kuziimarisha na pia kufanya nyasi zako ziote na kukua kwa haraka.


Zingatio: Kama udongo wako si imara kuhifadhi maji basi hakikisha unatandika plastiki maalum katikati ili kuepusha hasara ya upotevu wa maji mara kwa mara.


⥈BWAWA LA SIMENTI

Kwa Bwawa la simenti unapaswa kufuata kanuni na taratibu hizi ili uweze kutengeneze bwawa zuri na lenye viwango:-

➧Chagua eneo zuri lenye sifa.

➧Fanya usafi wa eneo la kujengea bwawa lako (ondoa visiki na vikwazo vinginevyo).

➧Fanya vipimo kama ni bwawa la usawa wa ardhi basi vipimo vyake ni sawa na lile la udongo,vitatofautiana kwenye matumizi ya simenti,kokoto na maji. Kama ni kisima kwaajili
ya vifaranga kitaanzia usawa wa ardhi kwenda juu kwa 1m.


Kumbuka:Katika aina zote hizi za mabwawa usisau kuweka mabomba maalumu makubwa na yenye unene wa kutosha na imara kwaajili ya kuruhusu maji kuingia na kutoka, pia na mfuniko wa nyavu au waya ili kuzuia samaki kutoka wakati wa kubadilisha maji ama wakati wa uvunaji.

Pia usisahau kuweka shimo dogo litakalo kurahisishia wakati wa uvunaji.


        UANDAAJI WA BWAWA LA SAMAKI KWA AJILI YA KUPANDIKIZA SAMAKI


➧Kausha bwawa lako lote.

➧Weka madini (kemikali) kwa ajili ya kuuwa vijidudu acha likae kwa muda wa wiki moja.

➧Jaza maji bwawa lako (robo tatu ya bwawa).

➧Weka mbolea ya kuku kidogo kwenye kiroba kilichotobolewa matundu madogomadogo na juu kifunge na kamba, kitumbukize kiroba hicho ndani ya bwawa kwenye ukingo mmoja na uache kiroba hicho kwa siku kadhaa huku ukipima kiwango cha urutubisho wa bwawa lako (search disc ama mkono).

➧Ukiona ukijani umeshajaa wakutosha (usizidi sana) toa kiroba nje.

➧Pandikiza samaki wako kwa kutumia vipimo vya uwiano maalum kwa kupandikiza samaki kulingan na ukubwa wa bwawa.


FAIDA NA HASARA ZA UCHAGUZI WA AINA YA BWAWA LA KUFUGIA SAMAKI


 Bwawa lililosakafiwa na Udongo wa     Mfinyanzi

Faida zake:

 Mkulima anapunguza gharama ya ulishaji (samaki hupata chakula cha asili ndani ya bwawa).

 ➧Gharama ndogo za ujenzi.

 ➧Uzalishaji mkubwa wa hewa safi.

 ➧Kiwango cha joto si kikubwa.


Hasara zake:

Uimara (sio imara zaidi ukilinganisha na bwawa la simenti).


  
                 Bwawa lililosakafiwa na Simenti

Faida zake:

Ni imara.

Hasara zake:

➧Samaki wanategemea zaidi chakula toka kwa mfugaji (uzalishaji wa chakula cha asili ni hafifu).

➧Gharama za kulitengeneza ni kubwa pia lina mahitaji mengi zaidi.

➧Pia kiwango cha joto wakati wa jua kali huzidi (hivyo  humpa mkulima gharama ya kununua               mashine ya kuzalishia hewe safi ndani ya maji).



  Uchimbaji wa bwawa la kufugia samaki inasisitizwa kuwa ni vizuri ukazingatia maelezo ya kitaalamu katika uchimbaji wa bwawa ili uweze kufanikiwa katika kazi hii ya ufugaji wa samaki na kupata mavuno mengi zaidi ya samaki ukiwa na bwawa imara.