Sunday 13 January 2019

UFUGAJI WA KAA MATOPE KWA KUTUMIA NJIA ZA ASILI AU KIENYEJI

 UFUGAJI WA KAA MATOPE

MUD CRAB FATTENING






  Ufugaji huu wa kaa ni moja kati ya ufugaji uliosahaulika Tanzania.Aina hii ya kaa hufugwa Zaidi na wakazi waishio pembezoni mwa vyanzo vikubwa vya maji vya asili zaidi waishio pembezoni mwa bahari.Kaa matope(mud crab) kwa asili hupenda eneo lenye matope hivyo hata ufugaji wake hufanyika ndani ya eneo lenye mikoko pembezoni mwa bahari,kwa kawaida eneo lenye miti ya mikoko aina ya udongo iliyotawala ni  tope zito.

 NJIA ZA UFUGAJI WA KAA MATOPE 
              
>>Kwa kawaida kuna njia kuu mbili za kienyeji                  zinazotumika   kufugia kaa matope;

      1) Njia ya kutenga vyumba kwa kutumia vipande vya mianzi/Vizimba vya mianzi(bamboo cages).

        2) Njia ya kutenga  bwawa maalumu la kutumia vipande vya mianzi (Mud crab bamboo pen  culture). 
                                     

     NJIA YA KUTENGA VYUMBA KWA KUTUMIA VIPANDE VYA                             MIANZI/VIZIMBA VYA MIANZI                                          (BAMBOO CAGES)

  
   Aina hii ya ufugaji mfugaji hupaswa kutengeneza kizimba kikubwa na kukigawanya katika vyumba vidogo vidigo ambapo ndipo watakapoishi kaa hao/Baadhi ya wafugaji huweka kaa moja mpaa wawili ndani ya chumba kimoja.

  Ukubwa wa kizimba kikubwa unaweza kuwa mkubwa kulingana na uambuzi wa mfugaji na eneo alilo nalo japo urefu uwe kati ya m1.60 - m1.83, lakini ukubwa wa vyumba ya ndani unatakiwa usivibane sana itawaathiri katika ukuaji wao,kwa kawaida inatakiwa kwa kila chumba kimoja kiwe na urefu usiopungua cm 92 na upana usiopungua cm23.Ufuniko wa juu unaacha na uwazi mdogo kwaajili ya kulishia na kupata hewa ya kutosha(uwazi kati ya kipande cha mti moja na mwingine).
                                   

      MUONEKANO WA NJIA YA KUTENGA VYUMBA KWA KUTUMIA VIPANDE VYA  MIANZI/VIZIMBA VYA MIANZI          (BAMBOO CAGES)                    




        Baadhi ya faida za njia ya vizimba ya kutenga vyumba       ukilinganisha na bwawa la mianzi:


      *Njia hii inapunguza ugombaniaji wa chakula na mahitaji  mengine kutokana na kwamba kila chumba kina idadi ndogo  sana ya kaa.

      *Lakini pia njia hii inapunguza uwezekano wa kaa   kupigana,kupeana majeraha baina ya kaa wakubwa na
     wadogo.

                 Udhaifu wake:

        *Inatumia miti mingi kwenye ujenzi wake.


  Njia ya kutenga  bwawa maalumu la kutumia vipande vya mianzi (Mud crab bamboo pen culture):

      Hii ni njia rahisi Zaidi,haitofautiani sana na njia iliyopita,utofauti wa njia hii ni kwamba hakuna mgawanyo wa vyumba   na mianzi iliyojengewa pembezoni hujengwa katika mfumo wa kulalia ndani ya bwawa na si kusimamisha wima,pia juu halifunikwe.Mianzi hulazwa kwa ulalo wa nyuzi 450.

      Lengo la kulaza mianzi hii ni kuzuia Kaa kupanda juu na kukimbia nje toka ndani ya bwawa,kutokana na uzito wa kaa na utelezi wa mti wa aina ya mianzi kaa hawezi kupanda juu na kutoka nje kwenye bwawa la aina hii.

     Kwa kawaida kaa matope (mudcrab) ana tabia ya kupendelea kutoroka nje ya kizimba ama bwawa kwaajili ya kwenda kutaga kwenye kina kirefu kati ya mita 200,mazingira haya ndio yenye hali joto na chuvi ya kiwango kizuri kwa ukuaji na upatikanaji wa chakula cha watoto wa kaa wakiwa wadogo sana na zaidi na baadae wakifikia hatua ya vifaranga wanahama na kurudi sehemu yenye tope na mchanganyiko wa maji chumvi na baridi (brackishwater kwaajili ya ukuaji) hali hii ndio inayowafanya wawe wa kipekee na vigumu kwa wao kufugwa na kuzalishwa majumbani (difficult tu breed and culture mudcrab in captivity) ,pia hupendelea kutoka nje kwaajili ya kutafuta chakula(kaa anakula mabaki ya vitu vingi kama mabaki ya samaki walio kufa,mollusca,chaza na konokono bahari pamoja na mabaki ya maozea ya mimea ya majini,japokuwa kwa wafugaji wa kienyeji huwalisha hata mabaki ya vyakula toka majumbani kama vile ugali na vinginevyo kwani kaa huwa si mchaguzi sana wa vyakula).


   Muonekano wa njia ya kutenga bwawa maalumu la kutumia vipande vya mianzi 
          (Mud crab bamboo pen culture)







   Baadhi ya Faida za Njia ya kujenga  bwawa maalumu la kutumia vipande vya mianzi (Mud crab bamboo pond):
  
        *Haitumii miti mingi hivyo ina faida kiuchumi na kimazingira pia.

    Udhaifu wake: 
  
I   *Inaruhusu kaa kupigana na kutoana majeraha wakati wa kugombania chakula na kuwadhoofisha kaa wadogo kuwa anyone na kuathirika kiukuaji.
     Njia hizi mbili zote hufanyika eneo la ufukweni kwenye matope hasahasa chini ama pembezoni mwa miti aina ya mikoko eneo lenye maji kati ya mita 1 mpaka mita 2, eneo hili pia ndilo eneo lenye uwepo wa chakula kingi kwa kaa kwani ndilo eneo la mazalia ya samaki wengi na amaki wengi wadogo,konokono bahari,chaza na viumbe wengine  hupatikana kwenye maeneo haya.



                                      Faida za ufugaji wa Kaa matope

     *Ni moja kati ya ufugaji wa kipekee kutokana na changamoto ya kushindikana kuzalishwakwa njia za kisasa majumbani hivyo huwafanya wafugaji wengi kuachana nao,hii inakupa faida kuwa na soko Zaidi kutokana na kutokuwa na wazalishaji wengi.

      *Lakini pia aina hii ya ufugaji ni nzuri kwakuwa kaa endapo atalishwa vizuri na kuzingatia maelekkezo yote kaa huwa anachukua mda mfupi kukuwa na kuwa tayari kwaajili ya kuuzwa ama kwa matumizi,kwa kawaida kaa mdogo wa uzito kati ya grams 100 -175  ukamfuga anaweza kufikisha gram 250 – 350 kwa muda wa siku 15 – 20 tu.

     *Lakini faida nyingine ya aina hii ya ufugaji haina gharama kubwa kwa upande wa chakula,kaa si mchaguzi sana wa vyakula.

 *Pia faida nyingine kimazingira kaa anasaidia sana kwenye ikolojia kama mvunjavuja vyakula kwaajili ya wenzake(decomposer), pia ujenzi wake unatumia Zaidi vitu vya asili yaani mianzi ambayo inauwezo wa kuoza na kuisha hivyo haisababishi madhara kwenye viumbe wengine majini ni tofauti na plastic material kama plastic net na mabomba ya plastic na vinginevyo visivyoweza kuoza. 



No comments:

Post a Comment