Thursday 31 January 2019

BIDHAA MPYA KUTOKA A. A. S TANZANIA

   AAS sardines ni bidhaa yetu mpya ya dagaa wa ziwani walioandaliwa kwa kuzingatia afya na viungo asili,dagaa wetu wamekaangwa na viungo vifuatavyo:  
                         ⇝Tangawizi
                         ⇝Limao
                         ⇝Chumvi 

                         ⟿Kitunguu Saumu

             MUONEKANO WA BIDHAA YETU:-



BAADHI YA FAIDA ZA KIAFYA ZA DAGAAA NA VIUNGO VILIVYOTUMIKA KUANDAA DAGAA WA AAS: 

FAIDA KWA AFYA YA MOYO:

  Kama ilivyo kwa karanga na korosho,dagaa nao wameonesha kuwa na faida kubwa kwa wenye matatizo ya magonjwaya moyo. Dagaa wana virutubisho vingi na miongoni mwa virutubisho hivyo kunakiwango kikikubwa cha Omega-3 Fatty

Acids (EPA & DHA)
Katika tafiti nyingi za magonjwa ya moyo na tiba zake, virutubisho vya Omega 3 vimeonekana kuwa dawa au kinga kubwa sana ya magonjwa ya moyo. Chanzo kikuu cha virutubisho hivyo si vingine bali ni samaki pamoja na dagaa.

Aidha, dagaa pia ni chanzo kizuri cha Vitamin B12, ikiwa ni chanzo kizuri cha pili baada ya maini. Vitamin hii hufanyakazi kubwa ya kuboresha ustawi wa moyo na hivyo kuwa chakula kizuri cha kumpa ahueni au kinga madhubuti mlaji dhidi ya magonjwa ya moyo.

AFYA YA MIFUPA 

    Dagaa ni chanzo kingine kizuri cha madini ya Calcium' yenye jukumu la kuimarisha mifupa ya mwili, lakini pia kwenye dagaa kuna vitamin D ambayo huwa nadra sana kupatikana kwenye lishe.

Vitamin D hufanyakazi muhimu ya kuimarisha afya ya mifupa kwani ndiyo inayosaidia unyonywaji mwilini wa madini ya calcium'. Vile vile dagaa ni chanzo kizuri cha madini aina ya phosphorus',ambayo nayo huimarisha mifupa.

DAGAA NA MARADHI YA KANSA 

    Kwa miaka mingi, watafiti wameona jinsi ambavyo dagaa inavyoweza kudhibiti seli zinazosambaza saratani mwilini. Hivyo imethibitika pasi na shaka kuwa virutubisho vilivyomo kwenye dagaa huweza kutoa kinga kubwa dhidi ya ugonjwa wa saratani.


WAMEJAA PROTINI

   Kama una upungufu wa protini mwilini,basi kula dagaa kwani wao wana kiwango kikubwa cha kirutubisho hicho.Protini husaidia uzalishaji wa Amino acids' ambazo ni muhimu kwa uzalishaji wa chembe hai mwilini na uimarishaji wa mfumo wa kinga ya mwili (body immune system). 

Hizi ni baadhi tu ya faida zake na nyingine nyingi ambazo hazikuainishwa zipatikanazo kwenye viungo vilivyotumika kama tangawizi,vitunguu saumu na limao. 

TAHADHARI:

  Wagonjwa wa figo na wale wenye matatizo ya ;gout', wanashauriwa kula dagaa kiasi kidogo na kwa tahadhari kubwa au kuepuka kabisa. Sababu inayotolewa ni kwamba, kama ilivyo kwa baadhi ya vyakula vingine, dagaa huwa na vitu (purine) ambavyo vinaweza kuwasumbua watu wenye magonjwa hayo, vinginevyo dagaa siyo chakula cha kukosa kula! 

Chanzo: M.Mkavu (Mtaalamu wa tiba lishe Tanzania)


No comments:

Post a Comment