Thursday 28 February 2019

UJENZI WA BWAWA LA KUFUGIA SAMAKI

UJENZI BORA WA BWAWA LA SAMAKI

   Ni jambo muhimu sana kuchagua eneo zuri kwa ajili ya ujenzi wa bwawa la samaki ili kufanikisha na kurahisisha kwa urahisi kazi ya kufuga samaki. Si kila eneo la ardhi hufaa kwa kazi ya kufuga samaki. 

 Bwawa linaweza kuchimbwa kwa mkono au kwa mashine, njia zote mbili ni sahihi isipokuwa kama bwawa ni kubwa au unakusudia kufuga kibiashara ni vema ukatumia mashine kwa sababu mashine inafanya kazi kwa haraka na hivyo kumaliza mapema, pia ufanisi wake unakuwa ni mkubwa ukilinganisha na na ufanisi wa bwawa linalochimbwa kwa mkono.

                                             Ujenzi wa Bwawa la Samaki

             SIFA ZA ENEO LA KUJENGA BWAWA LA KUFUGIA SAMAKI


Kwa Bwawa la kusakafiwa kwa udongo wa mfinyanzi hizi ni baadhi ya sifa muhimu sana za kuzingatia katika chaguzi sahihi la eneo:-


➧Liwe karibu na chanzo cha maji salama.

➧Liwe kwenye eneo lenye udongo wa mfinyanzi kwa sababu hauruhusu maji kunywea kirahisi.

➧Liwe katika eneo lenye mteremko kidogo (si lazima sana) ili uwezeshe maji kutiririka kutoka na kuingia bwawani.


Kwa Bwawa la kusakafiwa kwa simenti hizi ni baadhi ya sifa pia muhimu sana za kuzingatia katika ujenzi katika eneo husika:-


➧Liwe na karibu na chanzo cha maji salama.

➧Liwe katika eneo lenye udongo wa mfinyanzi (si lazima sana), uwiano kati ya mchanganyo wa simenti,mchanga na maji wakati wa kutengeneza bwawa la samaki lililo sakafiwa kwa simenti.
            
➧Ni muhimu sana kwa kiwango cha simenti,kokoto kuwa kikubwa zaidi ya kiwango cha                       mchanga na maji ili kuepukana na tatizo la bwawa kupoteza maji kwa mda mfupi.


       KANUNI NA TARATIBU ZA UTENGENEZAJI WA BWAWA LA KUFUGIA SAMAKI

 Ili uweze kufanikwa katika ujenzi bora wa bwawa la kufugia samaki unapaswa kufuata kanuni na taratibu zote katika ujenzi huo.

⥈BWAWA LA UDONGO

Kwa Bwawa la udongo unapaswa kufuata kanuni na taratibu hizi ili uweze kutengeneze bwawa zuri na lenye viwango:-

➧Chagua eneo zuri lenye sifa.

➧Pima udongo.

➧Pima maji.

➧Fanya usafi wa eneo la kujengea bwawa lako (ondoa visiki na vikwazo vinginevyo).

➧Fanya vipimo vya ukubwa wa bwawa lako kulingana na mahitaji yako na ukubwa wa eneo                 lako.
           
➧Zingatia unapofanya vipimo kumbuka kwa kila sqm 1ya bwawa lako utapandikiza samaki                    watatu.

                                     
 Pandikiza majani ya kutosha kwenye kuta.kingo na migongo ya bwawa lako ili kuimarisha bwawa lako lisiharibike kirahisi na mmonyoko wa udongo. Hakikisha unashindilia vizuri kuta,kitako na migongo ya bwawa lako (tumia vitu vizito vya kushindilia ili kuiamarisha zaidi).

 Zoezi hili litafanywa kwa muda wa wiki mbili mpaka tatu likiambatana na zoezi la kumwagilia maji kwa kiasi kidogo sana kwenye kuta ili kuziimarisha na pia kufanya nyasi zako ziote na kukua kwa haraka.


Zingatio: Kama udongo wako si imara kuhifadhi maji basi hakikisha unatandika plastiki maalum katikati ili kuepusha hasara ya upotevu wa maji mara kwa mara.


⥈BWAWA LA SIMENTI

Kwa Bwawa la simenti unapaswa kufuata kanuni na taratibu hizi ili uweze kutengeneze bwawa zuri na lenye viwango:-

➧Chagua eneo zuri lenye sifa.

➧Fanya usafi wa eneo la kujengea bwawa lako (ondoa visiki na vikwazo vinginevyo).

➧Fanya vipimo kama ni bwawa la usawa wa ardhi basi vipimo vyake ni sawa na lile la udongo,vitatofautiana kwenye matumizi ya simenti,kokoto na maji. Kama ni kisima kwaajili
ya vifaranga kitaanzia usawa wa ardhi kwenda juu kwa 1m.


Kumbuka:Katika aina zote hizi za mabwawa usisau kuweka mabomba maalumu makubwa na yenye unene wa kutosha na imara kwaajili ya kuruhusu maji kuingia na kutoka, pia na mfuniko wa nyavu au waya ili kuzuia samaki kutoka wakati wa kubadilisha maji ama wakati wa uvunaji.

Pia usisahau kuweka shimo dogo litakalo kurahisishia wakati wa uvunaji.


        UANDAAJI WA BWAWA LA SAMAKI KWA AJILI YA KUPANDIKIZA SAMAKI


➧Kausha bwawa lako lote.

➧Weka madini (kemikali) kwa ajili ya kuuwa vijidudu acha likae kwa muda wa wiki moja.

➧Jaza maji bwawa lako (robo tatu ya bwawa).

➧Weka mbolea ya kuku kidogo kwenye kiroba kilichotobolewa matundu madogomadogo na juu kifunge na kamba, kitumbukize kiroba hicho ndani ya bwawa kwenye ukingo mmoja na uache kiroba hicho kwa siku kadhaa huku ukipima kiwango cha urutubisho wa bwawa lako (search disc ama mkono).

➧Ukiona ukijani umeshajaa wakutosha (usizidi sana) toa kiroba nje.

➧Pandikiza samaki wako kwa kutumia vipimo vya uwiano maalum kwa kupandikiza samaki kulingan na ukubwa wa bwawa.


FAIDA NA HASARA ZA UCHAGUZI WA AINA YA BWAWA LA KUFUGIA SAMAKI


 Bwawa lililosakafiwa na Udongo wa     Mfinyanzi

Faida zake:

 Mkulima anapunguza gharama ya ulishaji (samaki hupata chakula cha asili ndani ya bwawa).

 ➧Gharama ndogo za ujenzi.

 ➧Uzalishaji mkubwa wa hewa safi.

 ➧Kiwango cha joto si kikubwa.


Hasara zake:

Uimara (sio imara zaidi ukilinganisha na bwawa la simenti).


  
                 Bwawa lililosakafiwa na Simenti

Faida zake:

Ni imara.

Hasara zake:

➧Samaki wanategemea zaidi chakula toka kwa mfugaji (uzalishaji wa chakula cha asili ni hafifu).

➧Gharama za kulitengeneza ni kubwa pia lina mahitaji mengi zaidi.

➧Pia kiwango cha joto wakati wa jua kali huzidi (hivyo  humpa mkulima gharama ya kununua               mashine ya kuzalishia hewe safi ndani ya maji).



  Uchimbaji wa bwawa la kufugia samaki inasisitizwa kuwa ni vizuri ukazingatia maelezo ya kitaalamu katika uchimbaji wa bwawa ili uweze kufanikiwa katika kazi hii ya ufugaji wa samaki na kupata mavuno mengi zaidi ya samaki ukiwa na bwawa imara.


Wednesday 27 February 2019

CHAKULA CHA SAMAKI

CHAKULA CHA SAMAKI NA ULISHAJI WAKE

         
   Kuna aina mbalimbali ya vyakula vya samaki vinavyotengenezwa kwa mchanganyiko wa vitu mbalimbali vyenye virutubisho vyote muhimu vinavyohitajika na samaki husika kulingana na umri wake na aina yake.

   Mfano: Chakula cha wazazi na watoto huwa na kiwango kikubwa cha protini ili kuwasaidia wazae watoto wengi ndani ya wakati, lakini  pia kuwasaidia watoto waweze kukua kwa haraka na ufasaha.

Kwa utaalamu vyakula hivi hutokana na mchanganyiko wa vitu kama:

Maharage, dagaa,pumba za mpunga na za mahindi, mtama,vitamin mix,madini na vingine vingi ambavyo husagwa na kuchanganywa kwa pamoja kwa kiwango maalumu kilingana na aina ya samaki anayeenda kulisha pia na umri wake. 

Baada ya hapo chakula hiki kama ni cha samaki wa kubwa ama vifaranga wakubwa kidogo basi kitatengenezwa kuwa katika mfumo wa tambi inayoelea na kuanikwa vizuri kwenye kivuli ili kikauke.

Kama ni cha watoto wadogo basi kiache katika mfumo wa poda tu. Kikisha kauka kabisa kihifadhi kwenye mifuko maalumu ili kisiharibike.

   Muhimu:Usianike chakula kwenye jua utapoteza virutubisho.


UHIFADHI WA CHAKULA CHA SAMAKI

Baadhi ya njia na mazingira ambayo unayoweza kuhifadhi chakula cha samaki: 

➧Baada ya kutengeneza chakula hifadhi kwenye vifuko vidogo maalumu.

➧Tengeneza kichanja kidogo chenye urefu wa nusu mita na tandika vifuko hivyo vyenye chakula           juu ya kichanja.

➧Kichanja kiwe ndani ya chumba chenye kuruhusu mzunguko wakutosha wa hewa safi ili kuepuka      chakula chako kisiharibiwe na bakteria wanaozaliana kwenye joto na unyevunyevu.

➧Kama una chakula kingi sana kichanja chaweza kuwa kwenye ghorofa zaidi moja au mbili, la            msingi ni kuacha nafasi ya kutosha kati ya ghorofa moja na ingine ili kuruhusu hewa yakutosha          kupita.
  
                   
 JINSI YA KULISHA SAMAKI NA MDA SAHIHI WA KULISHA SAMAKI

  Watu wengi hukosea mda sahihi wa kulisha samaki na hivyo kuathiri afya na ukuaji wa samaki kiujumla. Je ni muda gani sahihi wa kulisha samaki chakula?

 ➧Kitaalamu inashauriwa ulishe samaki wako asubuhi kati ya saa kumi na mbili mapaka saa moja na nusu na kwa muda wa jioni kati ya saa kumi na moja na nusu mpaka saa kumi na mbili na nusu.

Mda huu unapendekezwa kwa sababu kunakuwa hamna joto kali sana, wakati wa joto sana hasa mda kama wa mchana shughuli za ndani ya mwili huongezeka pia, samaki upoteza hamu ya kula hivyo haishauriwi kulisha mda huo.

Jinsi ya kulisha samaki

➧Kitaaalamu samaki hupaswi kumlisha kwa makadirio, inatakiwa uchukue sampuli ndogo ya    samaki toka kwenye bwawa lako halafu uwapime uzito na urefu, pia ujue ukubwa wa bwawa lako.
    
➧Kienyeji hasa kwa wakulima wadogo,unaweza kukadiria kwa kupima kiganja chako na                  kuwatupia kwenye bwawa.

 Zingatia: Tumia eneo moja tu la kuwalisha samaki wako kila siku,kama umeamua kuchagua  kona moja ya bwawa hakikisha unatumia hiyo kila siku.

    Uhifadhi mzuri wa chakula cha samaki na ulishaji bora wa samaki kwa kuzingatia kanuni kunaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa mafanikio ya uzalishaji wa samaki kwa kiwango kikubwa endapo utafuata taratibu na kanuni za kulisha samaki na uchaguzi mzuri wa  chakula bora cha samaki.


Tuesday 26 February 2019

AINA ZA MABWAWA YA KUFUGIA SAMAKI

FAHAMU AINA KUU ZA MABWAWA YA KUFUGIA SAMAKI 

 

                     Kuna aina kuu mbili za mabwawa:


                       1. Bwawa la Udongo

                      2. Bwawa la Simenti                                                                          

1.(a)Bwawa la udungo husakafiwa na udongo wa mfinyanzi unaohifadhi maji kwa mda mrefu bila kuruhusu upotevu wa maji ardhini.

                                                        
b)Bwawa la udongo lililotandikwa karatasi maalumu ya plastic:

Kwa eneo lisilokuwa na udongo mzuri unaoweza kuhifadhi maji kwa muda mrefu ni vizuri ukatengeneza aina hii ya bwawa ili kuepusha hasara ya upotevu wa maji mara kwa mara.

                            
Hizi ni Baadhi ya faida na hasara za bwawa la udongo:

Faida:

➧Hupunguza gharama za ulishaji kwa mfugaji kwakua samaki hujipatia chakula cha asili ndani ya bwawa.

➧Gharama zake za ujenzi ni ndogo ukilinganisha na bwawa la simenti. 

➧Halihitaji ujuzi mkubwa sana wa ujenzi ukilinganisha na bwawa la simenti. 

➧Gharama za kukuza samaki kwa bwawa la udongo ni ndogo kwakua ndani ya bwawa la udongo kunauzalishwaji mkubwa wa hewa safi pia kiwango cha joto si kikubwa hasa kwa bwawa la udongo wa ufinyanzi lisilokuwa na plastic hivyo huwafanya samaki wakue vizuri na kwa haraka na bia humpunguzia mfugaji gharama za ziada za kununua vizalishaji hewa(aerator). 

Hasara:

➧Sio imara sana ukilinganisha na bwawa la siment. 

➧Usipokua makini wakati wa uchaguzi sahihi wa eneo la ujenzi wa bwawa lenye udongo unaohifadhi maji vizuri unaweza pata hasara ya upotevu wa maji mara kwa mara.


2. Bwawa la simenti hili husakafiwa kwa simenti na hutengenezwa kwa tofali,simenti,kokoto,nondo na matirio mengine.Ujenzi wa bwawa hili kidogo ni wagharama ukilinganisha na bwawa la udongo kwakuwa linahitaji vifaa vingi zaidi. 


FAHAMU AINA KUU ZA MABWAWA YA KUFUGIA SAMAKI  

                     Kuna aina kuu mbili za mabwawa:


                       1. Bwawa la Udongo

                      2. Bwawa la Simenti                                                                          

1.(a)Bwawa la udungo husakafiwa na udongo wa mfinyanzi unaohifadhi maji kwa mda mrefu bila kuruhusu upotevu wa maji ardhini.

                                                     


(b)Bwawa la udongo lililotandikwa karatasi maalumu ya plastic:

Kwa eneo lisilokuwa na udongo mzuri unaoweza kuhifadhi maji kwa muda mrefu ni vizuri ukatengeneza aina hii ya bwawa ili kuepusha hasara ya upotevu wa maji mara kwa mara.

                            



Hizi ni Baadhi ya faida na hasara za bwawa la udongo:

Faida:

➧Hupunguza gharama za ulishaji kwa mfugaji kwakua samaki hujipatia chakula cha asili ndani ya bwawa.

➧Gharama zake za ujenzi ni ndogo ukilinganisha na bwawa la simenti. 

➧Halihitaji ujuzi mkubwa sana wa ujenzi ukilinganisha na bwawa la simenti. 

➧Gharama za kukuza samaki kwa bwawa la udongo ni ndogo kwakua ndani ya bwawa la udongo kunauzalishwaji mkubwa wa hewa safi pia kiwango cha joto si kikubwa hasa kwa bwawa la udongo wa ufinyanzi lisilokuwa na plastic hivyo huwafanya samaki wakue vizuri na kwa haraka na bia humpunguzia mfugaji gharama za ziada za kununua vizalishaji hewa(aerator). 

Hasara:

➧Sio imara sana ukilinganisha na bwawa la siment. 

➧Usipokua makini wakati wa uchaguzi sahihi wa eneo la ujenzi wa bwawa lenye udongo unaohifadhi maji vizuri unaweza pata hasara ya upotevu wa maji mara kwa mara.


2. Bwawa la simenti hili husakafiwa kwa simenti na hutengenezwa kwa tofali,simenti,kokoto,nondo na matirio mengine.Ujenzi wa bwawa hili kidogo ni wagharama ukilinganisha na bwawa la udongo kwakuwa linahitaji vifaa vingi zaidi. 

Baadhi ya faida na hasara za ujenzi wa bwawa la siment:

Faida:

➧Ni imara,hudumu kwa muda mrefu ukilinganisha na bwawa la udongo.

Hasara:

➧Utengenezwaji wake ni wa gharama zaidi ukilinganishasa na bwawa la udongo,linatumia vifaa vingi na vya gharama.

➧Pia linahitaji utaalamu zaidi wa usimamizi wakati wa ujenzi.

➧Ndani ya bwawa la simenti uzalishwaji wa chakula cha asili,hewa safi huwa mdogo ukilinganisha na bwawa la udongo hivyo humuongezea mkulima gharama za ulishaji.

➧Hatari ya mabadiliko ya kiwango cha joto ndani ya bwawa la simenti na lile lililo tandikiwa karatasi ya plastic huwa ni makubwa na hutokea mara kwa mara ukiliganisha na bwawa la udongo hivyo huathiri ukuaji na maisha ya samaki. 


Visima kwaajili ya kuhifadhia samaki wazazi na vifaranga wadogo:

Pia kuna visima maalum kwaajili ya kuhifadhia samaki wakubwa wazazi ama samaki wadogo (vifaranga).

                            

Baadhi ya faida na hasara za ujenzi wa bwawa la siment:

Faida:

➧Ni imara,hudumu kwa muda mrefu ukilinganisha na bwawa la udongo.

Hasara:

➧Utengenezwaji wake ni wa gharama zaidi ukilinganishasa na bwawa la udongo,linatumia vifaa vingi na vya gharama.

➧Pia linahitaji utaalamu zaidi wa usimamizi wakati wa ujenzi.

➧Ndani ya bwawa la simenti uzalishwaji wa chakula cha asili,hewa safi huwa mdogo ukilinganisha na bwawa la udongo hivyo humuongezea mkulima gharama za ulishaji.

➧Hatari ya mabadiliko ya kiwango cha joto ndani ya bwawa la simenti na lile lililo tandikiwa karatasi ya plastic huwa ni makubwa na hutokea mara kwa mara ukiliganisha na bwawa la udongo hivyo huathiri ukuaji na maisha ya samaki. 


Visima kwaajili ya kuhifadhia samaki wazazi na vifaranga wadogo:

Pia kuna visima maalum kwaajili ya kuhifadhia samaki wakubwa wazazi ama samaki wadogo (vifaranga).