Friday 21 December 2018

UFUGAJI WA SAMAKI KWA KUTUMIA NJIA ZA KISASA ZINAZOZINGATIA UHIFAHDI MAZINGIRA, KATIKA ENEO DOGO NA GHARAMA NAFUU:



Ndugu mfuatiliaji wa fululizo za masomo ya AAS ufugaji wa samaki ni teknolojia inayokuwa kwa kasi sasa katika nchi yetu pia yaweza kuwa ni njia moja wapo itakayosaidia katika juhudi za kutunza mazingira,kukuza kipato na pia kuunga mkono juhudi za Raisi wetu wa awamu ya Tano Dr. John Joseph Pombe Magufuli za kuelekea katika uchumi wa viwanda.

Leo tutajifunza aina za ufugaji wa samaki kwa njia za kisasa na za gharama nafuu pia zinazingatia uhifadhi wa mazingira (aina hii ya ufugaji ni rahisi hata kwa Mtanzania mwenye eneo dogo,anayeishi katikati ya mji anaweza kufuga bila shida yeyote):

UFUGAJI WA SAMAKI KWA KUTUMIA MABWAWA TURBAI YA PLASTIC/MABWAWA YANAYO HAMISHIKA:
 
Aina hii ya ujenzi wa mabwawa hutengenezwa kwa kutumia turbai maalumu za plastic pamoja na pomba za chuma zinazopindwa na kutengenezwa kuwa katika umbo la mraba ama mstatili,mabomba haya huwa na ukubwa tofauti ili yaweze kuvaana kirahisi na kutoa umbo la bwawa na kuchomolewa kirahis wakati wakuhama ili kumrahisishia mfugaji kutokufungwa kufanya kazi sehemu moja.Aina hii ya mabwawa ujenzi wake na ufungwaji wake wa mabomba unafanana sana na ufungwaji wa mahema.

MUONEKANO WA BWAWA LA KUHAMISHIKA:

 


FAIDA ZA UJENZI HUU WA MABWAWA:
 
    Yana gharama nafuu kwa upande wa ujenzi hivyo humsaidia mfugaji kutumia gharama ndogo katika ujenzi.Hapa mfugaji hatakuwa na gharama za kununua cement,nondo,kokoto,mchanga wala kutafuta mashine za kuchimba,anachotafuta ni bomba za chuma na turbai nzito ya plastic basi.

    Yanazingatia uhifadhi wa mazingira,hapa mfugaji hatachimba ardhi kwani yenyewe huanzia juu ya uso wa ardhi,pia kama ni mfugaji anayetumia kemikali katika ufugaji wake kwenye chakula ama kutibu samaki basi aina hii ya mabwawa inakinga kemikali zile kudhuru ardhi na viumbe wengine waishio arhini (Angalizo ili kutimiza hili pindi tu mfugaji anapoona plastic sheet imechakaa na anataka kubadii nyingine anapaswa kuzingatia sana utupaji wa mifuko hiyo sehemu sahihi na si kuiacha izagae ovyo,ni mbaya kwenye mazingira,ni vyema akaikusanya na kuiweka sehemu moja ili iunganike na takataka nyingine kwaajili ya matumizi mengine ama kufanyiwa recycling)

    Faida nyingine ya mabwawa haya huruhusu ufugaji kufanyika katika eneo dogo  kwa unadhifu Zaidi.Hii hufungua fursa ya ufugaji wa samaki kwa wakazi waishio katikati ya miji wenye maeneo madogo.


UDHAIFU WA UJENZI HUU WA MABWAWA:
  Mfugaji asipokua makini wakati wa uchaguzi wa turbai anaweza pata turbai zilizo chini ya kiwango na kuleta usumbufu wa kupasuka na kuvujisha maji mara kwamara.

   Pia plastic ina sifa ya kupata joto sana wakati wa jua kali hivyo kwa wafugaji waishio maeneo ya joto  akiwa amepandikiza samaki wengi kupitiliza ndani ya eneo dogo joto liliongezeka samaki wataathirika,ni muhimu kama ni mfugaji wa maeneo ya joto awe makini kufuatilia mabadiliko ya hali joto ya maji kwa kupima temperature mara kwa mara ili aweze kuzuia athari hizi.

USHAURI KWA WAFUGAJI WANAOISHI VIJIJINI,PEMBEZONI MWA HIFADHI ZA BAHARI NA HIFADHI ZA WANYAMA PORI NA MAZINGIRA KWA UJUMLA:
 
Kwa matokeo chanya ya ufugaji wako na pasipo kuleta uharibifu wa mazingira ni vizuri kutumia ufugaji huu katika hali ya ufugaji mseto (intergrated fish farming)  kwani utakupa faida kubwa kwakua ufugaji huu mseto unaleta mtegemeano mkubwa wa kiikolojia pia hautaaribu mazingira.
Mtegemeano wa kiikolojia unaotokea:
Unapofuga kuku ama bata pamoja na samaki kinyesi cha kuku ama bata utakitumia kutengenezea chakula cha asili kwenye bwawa(algae,phytoplankton,zoo plankton) lakini pia wakati wakubadili maji kwenye bwawa badala ya kumwaga maji ovyo,maji hayo kumbuka yana virutubisho vingi,mbolea nyingi ambayo ni nzuri sana kwenye ukuaji wa mimea hivyo unaelekezea bomba la outlet kwenye bustani yako yaweza kuwa ya mbogamboga,matunda,nafaka kama mahindi ama miti ya a mbao ambavyo vitakupa faida ya chakula pia na fedha,Zaidi ya hapo unapo vuna mazao yako kama mahinndi mabaki ya majani na magunzi hautatupa utawapatia mifugo yako kama nguruwe na wengineo hii itakusaidia kuepukana na migogoro ya kuachia mifugo ovyo kwenda ndani ya maeneo ya hifadhi lakini pia itakusaidia katika utunzaji mazingira kwani utajikuta hautaacha takataka ama mabaki yeyote ovyo kwenye mazingira,kila kitu kinakuwa na matumizi yake kwa mtegemeano huo wa kiikolojia ya viumbe uliyoitengeneza.   


Ahsante kwa kufuatilia masomo yetu,kwa msaada wowote usisite kuwasiliana nasi.